MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA MABALOZI WA UGANDA, CUBA NA IRAN KWA NYAKATI TOFAUTI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan leo amekutana na Mabalozi kutoka nchi tatu kwa wakati tofauti ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais alianza kwa kukutana na Balozi Mpya wa Uganda hapa nchini Mhe. Richard T. Kabonero ambaye alifika kuonana na Makamu wa Rais kwa mara ya kwanza ambapo alitumia nafasi hiyo kujitambulisha.

Katika mazungumzo na Makamu wa Rais, Balozi Kabonero alizungumzia nia ni ya dhati ya nchi yake katika kudumisha na kuimarisha uhusiano wa kindugu baina ya Tanzania na Uganda hasa ushirikiano wa kijamii, na kiuchumi ambapo tafiti za mafuta zinazoendelea katika ziwa Eyasi, mashirikiano ya sekta ya anga ili kusaidia kukuza utalii, mradi wa ujenzi ya reli ya kati na mradi wa umeme vijijini pamoja na kuanzishwa kwa jukwaa la biashara la sekta binafsi kutoka nchi husika ili kuweza kunufaika na fursa zitakazojitokeza baada ya kukamilika bomba la mafuta .

Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amewapongeza wananchi wa Uganda kwa kutimiza miaka 55 ya Uhuru.Pia aliipongeza Uganda kwa kutafiti na kugundua mafuta kwa kutumia wataalamu wazawa ambapo alisisitiza ushirikiano wa kitaalamu na wataalamu wa Tanzania.

Makamu wa Rais amemtakia heri na fanaka katika majukumu mapya ya Ubalozi wa Uganda hapa Tanzania na kumhakikishia ushirikiano wa Serikali.Makamu wa Rais alimalizia mazungumzo yake na Balozi huyo wa Uganda hapa nchini kwa kutoa shukrani zake za dhati kwa Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Museveni kwa ushirikiano wake walioutoa wakati wa ajali mbaya ya gari iliyowakuta Watanzania waliokuwa wanatoka Harusini ambapo watanzania 13 walifariki.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi mpya wa Uganda nchini Mhe. Richard T. Kabonero aliyefika ofisini kwa Makamu wa Rais kujitambulisha na kufanya mazungumzo, Ikulu jijini Dar es salaam. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja Balozi mpya wa Uganda nchini Mhe. Richard T. Kabonero mara baada ya kumaliza mazungumzo, Ikulu jijini Dar es salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkaribisha ofisini kwake Balozi wa Cuba nchini Mhe. Lucas Domingo Hernandez . (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Balozi wa Iran nchini Mhe. Moussa Farhang aliyefika ofisini kwa Makamu wa Rais kwa mazungumzo. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia kitabu chenye historia ya miji ya Iran ambacho alikabidhiwa na Balozi wa Iran nchini Mhe. Moussa Farhang aliyefika ofisini kwa Makamu wa Rais kwa mazungumzo. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).



from MICHUZI BLOG
via ZAMOTO MEDIA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini