MAMA ZAKHI A MEGHJI AFUNGUA MKUTANO WA 36 WA CHAMA CHA GIRL GUIDES & GIRL SCOUTS DUNIANI NCHINI INDIA

  Mjumbe wa Bodi ya  Udhamini ya Chama cha Tanzania Girl Guides (TGGA),  Mama Zakhia Meghji  akiwa na vioongozi wa Girl Guides na Girl Scouts wa Ulimwengu (WAGGGS) akiwasha mshumaa  kuashiria ufunguzi rasmi wa Mkutano Mkuu wa wa 36 wa WAGGGS nchini India. Meghji alimwakilisha Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan aliyepangwa kuwa mgeni rasmi kwenye mkutano huo wa kimataifa. Mama Samia ni Mlezi wa TGGA.
Mkutano huo hufanyika kila baada ya miaka mitatu na mara ya mwisho ulifanyika Honkong. Kuwashwa mshumaa ni  nuru ya moyo wa kujitolea katika juhudi za kuwafikia wasichana wengi zaidi popote walipo mjini na vijijini. Mkutano huo ulifanyika kuanzia Septemba 18 hadi 23 mwaka huu.

  Mama Zakhia Meghji  akiwa na Balozi wa Tanzania nchini India Mhe. Baraka Luvanda wakipambwa kwa nyimbo walipokuwa wakiingia ukumbini.
 Mjumbe wa Bodi ya  Udhamini ya Chama cha Tanzania Girl Guides (TGGA),  Mama Zakhia Meghji  akisoma hotuba wakati wa ufunguzi rasmi wa Mkutano Mkuu wa wa 36 wa WAGGGS nchini India.
 Waliokaa  kutoka kulia ni Balozi  wa Tanzania nchini India Mhe. Baraka Luvanda, Mama Zakhia Meghji, Mama Martha Qorro ambaye ni Mwenyekiti wa TGGA. Waliosimama wa pili kushoto ni  Aika wa Afrika Kusini,  kushoto kwake ni Maryam Mjema wa TGGA Kamishna wa Mambo ya Nje, Kamishna Mkuu wa TGGA, Symphorosa Hangi Nicola  Grinstead Mwenyekiti wa Bodi ya WAGGGS.


from MICHUZI BLOG
via ZAMOTO MEDIA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini