WAFANYAKAZI WA STAMICO WAPATA MAFUNZO YA UKIMWI

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.
SERIKALI imedhamiria kupambana na janga la Ukimwi ikiwa ni pamoja na kuandaa muongozo kwa wafanyakazi kupata elimu juu ya ugonjwa huo jinsi ya kujiepusha.

Hayo ameyasema Kaimu Mkurugenzi Masoko na Uwekezaji wa Shirika la Taifa la Madini (Stamico),  Aloyce Tesha wakati akifungua semina ya wafanyakazi wa shirika hilo katika kupata elimu ya Ukimwi pamoja na magonjwa sugu yasiyoambukiza , amesema semina hiyo ni muhimu kwa wafanyakazi katika kuweza kujikinga na magojwa ili waweze kutekeleza majukumu yao.

Tesha amesema kuwa wafanyakazi wakipata elimu wanaweza kufundisha familia zao pamoja na jamii zinazowazunguka katika uchukua tahadhari.

Amesema kuwa wafanyakazi wa shirika hilo wanakwenda sehemu mbalimbali za madini hivyo lazima wawe na elimu ya Ukimwi na magonjwa yasiyoambukiza.
 Afisa Mwitikio wa Taasisi za Umma kutoka Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dk. Hafidh Ameir akizungumza wakati akitoa mada ya Ukimwi katika semina wa wafanyakazi wa Stamico.
 Kaimu Mkurugenzi na Uwekezaji wa Stamico, Aloyce Tesha akizungumza katika ufunguzi wa semina ya wafanyakazi wa Stamico juu ya Ugonjwa wa Ukimwi na Magonjwa yasiyoambukiza leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wafanyakazi wakisiliza mada katika semina hiyo.
 Kaimu Mkurugenzi wa Masoko na Uwekezaji, Aloyce Tesha akiwa katika picha ya pamoja na wafanyazi wa stamico mara baada ya semina elimu ya ukimwi na Magonjwa yasiyoambukiza.

Sehemu ya kupimia ugonjwa wa kisukari. 


from MICHUZI BLOG
via ZAMOTO MEDIA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini