Facebook Kutumia Utafiti ili Kuboresha Habari Zake

Facebook Kutumia Utafiti ili Kuboresha Habari Zake
Kampuni ya facebook imetangaza kuwa imebadili kampuni inayoipa habari, ili kukabiliana na kile ilichotaja kama habari za uzushi na za kupotosha.

Afisa mkuu mtendaji wa kampuni hiyo ya facebook, Mark Zuckerberg, amesema mtandao wake sasa utakuwa ukiwauliza matumiaji wake ni vyanzo vipi vya habari wanaamini zaidi na hivyo kuwapa nafasi ya kwanza.

Waandishi wa habari wanasema kuwa kampuni hiyo ya facebook ambayo ina zaidi ya watumiaji bilioni mbili, inataka kusitisha usambazaji wa habari bandia na propaganda, baada ya mahusiano yaliyojawa na malumbano na mashirika ambayo yana misimamo mikali ya kisiasa.

Mapema mwezi huu, Mark Zuckerberg, alitangaza mabadiliko ya vyanzo vya habari ya kampuni hiyo, iliyonuiwa kuhimiza ujumbe zinazotumwa na familia na marafiki badala ya mashirika ya kibiashara na bidhaa.
Sponsored by ZAMOTO MEDIA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini