Mkurugezi kampuni iliyokuwa inaidai TFF yupo tayari kutoa ushahidi kesi ya Wambura

Mmoja wa wakurugenzi wa Jeksc Systems Limited iliyokuwa inaidai TFF Jost Rwegasira ameibuka na kuzungumzia kuhusu barua au nyaraka za kampuni hiyo zinazodaiwa zilighushiwa.

Rwegasira amesema yupo tayari kutoa ushahidi wake mahali popote endapo utaratibu wa yeye kufanya hivyo utafuatwa lakini kwa sababu tayari hukumu imeshatolewa hawezi kuweka jambo hilo hadharani labda ikitokea ameitwa mamlaka itakayokuwa ikisikiliza rufaa ya kesi hiyo.

“Uamuzi wa mahakama ya maadili umeshatoka, wametoa uamuzi bila kuuliza Jeksc. Nimefuatilia kila kitu tangu kilivyotangazwa lakini sina uwezo wa kuingilia mambo ya TFF lakini kwa kuwa uamuzi umeshatoka, kwa hiyo nilichonacho ni ushahidi kwa atakaekata rufaa au yule atakaekuwa anasikiliza rufaa.

“Naomba umma unielewe, wakati uamuzi umeshatolewa inamaana upande mmoja una uhakika na unachosema na upande wa pili unaopinga una uhakika kwa unachosema kwa hiyo mtu wa tatu atakaepelekewa rufaa kama itakuwepo ndiye mwenye mamlaka ya kumuomba mlalamikaji au mlalamikiwa kupeleka ushahidi.

“Naweza kutoa ushahidi kwa sharti moja, ni ipi barua inayolalamikiwa kwamba ni ya kufoji? Mimi sijaipata, siwezi kukaa pembeni nikatoa ushahidi kwamba hiyo barua sio ya kufoji mpaka wewe mwenye maswali uwe nayo uniulize barua hii unaijua?

“Jambo la pili kwa sababu unapinga hukumu ambayo ilishaotolewa, lazima uwe na ushahidi ambao umeombwa kutoa kwamba hii barua iliyoletwa kwenye kesi sisi tumeiona ni feki lakini kama sijaiona hiyo barua nina kubali nini au nakataa nini?

Shauri likienda mbele kwenye kamati ya maadili ya rufaa upo tayari kutoa ushahidi?

“Hata leo ukienda TFF wakakupa barua kwamba hii barua tuliyoletewa ni feki nipo tayari kuthibisha lakini katika press conference zote zilizotolewa nimeziangalia TFF hawajaonesha barua wanayoilalamikia sasa mimi nakubali au kukataa barua ipi? Ila ninachokubali ni kwamba nilikuwa mkurugenzi katika kampuni aliyoiendesha marehem lakni hiyo barua wanayolalamika imefojiwa naomba wailetwe kwanu mimi nipo tayari kuja kuiona halafu nithibitishe ndiyo au hapana.

Baada ya kufariki mkurugenzi mtendaji tulitangaza kampuni inasimamisha shughuli zake zote mpaka itakapotangazwa vinginevyo.
Sponsored by ZAMOTO MEDIA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini