Simba Baada ya Kutolewa kwenye Mashindano Kutua Leo Dar

Simba Baada ya Kutolewa kwenye Mashindano Kutua Leo DarBAADA ya kung’olewa katika michuano ya Kombe la Shirikisho, Simba wanatarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam, leo Jumatatu.

Simba inarejea Dar es Salaam kupitia Addis Ababa, Ethiopia na baada ya hapo wachezaji watakuwa na mapumziko mafupi.

Kikosi cha Simba kinatarajia kutua nchini saa 3:15 asubuhi kikitokea mjini Port Said, Misri ambako kilitoka sare ya bila kufungana na Al Masry na kung’olewa katika michuano ya Kombe la Shirikisho.

Simba iling’olewa kwa mabao ya ugenini iliyowapa Al Masry kwenye mchezo wa kwanza wa timu hizo jijini Dar es Salaam ulioisha kwa sare ya mabao 2-2.

Lakini juzi kwenye Uwanja wa Al Masry, Port Said nchini hapa, timu hizo zilitoka suluhu na Simba kuyaaga mashindano. Hata hivyo, vijana hao wa kocha Mfaransa, Pierre Lechantre walipoteza nafasi kadhaa ambazo zingeweza kuwapa bao na kusonga mbele.
Sponsored by ZAMOTO MEDIA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini