Wauza Dawa za Kulevya Kuanza Kuuwawa Marekani

Wauza Dawa za Kulevya Kuanza Kuuwawa Marekani
Matumizi ya dawa za kulevya bado ni gumzo kwa nchi mbalimbali duniani, jambo ambalo limekuwa likikabiliwa na nchi husika kwa kuweka sheria na adhabu zitakazo wajibisha wanaohusika na uuzaji na utumiaji.

Rais Donald Trump wa Marekani siku za hivi karibuni ametangaza kuwahukumu adhabu ya kifo watu wote watakaokutwa na hatia ya kuhusika na kuuza au kutumia dawa za kulevya.

Mpango huu wa Rais Trump umeelekezwa katika Idara ya Haki ya nchini humo kuwahukumu kifo madaktari, maduka ya dawa na watengeneza dawa ambao watakutwa wakijihusisha kwa namna yoyote ili na dawa za kulevya.

Inaelezwa kuwa Wamarekani zaidi ya Milioni 2.4 wamekuwa ‘mateja’ wa drugs, 42,000 waalikuwa kwa dawa hizo za kulevya mwaka 2016 na kujizidishia dawa imekuwa sababu iliyozoeleka ya vifo vingi nchini humo.
Sponsored by ZAMOTO MEDIA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini