Nimemjua Ruge miaka 20 iliyopita Dkt.Kikwete | ZamotoHabari

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

Rais wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Kikwete amesema kuwa alikuwa karibu sana kati ya Ruge Mutahaba pamoja na Joseph Kusaga.

Kikwete ameyasema hayo alipokuwa katika msiba wa uombolezaji wa Ruge Mutahaba aliyefariki juzi nchini Afrika Kusini alipokuwa anapatiwa matibabu.

"Nimekuwa karibu kati ya Ruge na Joseph Kusaga "Zaidi ya miaka 20 nimekuwa nao karibu kama mshauri nimewaunga mkono katika shughuli mbalimbali"amesema Kikwete.

Amesema angekuwa na uwezo wa kifedha ningewapa ili waende haraka.Dkt Kikwete Wakati akianzisha THT tulikuwa pamoja kwa sababu ya kuwa Rais niliwaunga mkono.

Aidha amesema alikuwa akifuatilia kwa karibu sana akiwa Hospitali.
Katika shughuli za siasa vyombo vya habari ni muhimu.Nilivyoandika kuwa kupoteza mzalendo limetoka kwa dhati kwa ajili ya Ruge

Ruge alifanya kwa kunufaisha wengi na tujitahidi kuishi kwa mfano wake alikuwa yu tayari kujitolea kwa ajili ya wengi tuwaombee ndugu na wanae waishi kama baba yao.Mwenyezi Mungu amjalie mapunziko mema amina.Hata walipokuwa wakitofautiana kati ya Ruge na Joseph Kusaga walikuwa wanakuja na kuwasuluhisha.
Rais wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Kikwete akizungumza na waandishi habari kuhusu Maisha aliyoyaishi aliyekuwa Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Vipindi wa Clouds Ruge Mutahaba

Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipoBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini