Daktari Awaonya Wanaume na Wanawake Kunyoa Nywele za Sehemu ya Siri | ZamotoHabari.

Daktari wa wanawake ameonya dhidi ya kunyoa sehemu za siri eti kama njia moja kudumisha usafi

Kulingana na Dkt Ignitius Kibe, Mungu aliumba binadumu awe na nywele hizo anapobalehe kwa sababu kadhaa na pia zina umuhimu sana hasa wakati wapenzi waposhiriki kitendo cha ndoa.

Akiwa kwenye mahojiano na runinga ya Citizen Jumatano Machi 27, daktari huyo alisema nywele hizo husaidia sana wakati wa kitendo cha ndoa.

Aidha, daktari huyo alisema sio salama kuzinyoa kwani mtu anaweza pata vipele na michubuko kwenye sehemu za siri

" Mimi kwangu binafsi napendelea hizo nywele ziwepo, zina umuhimu sana wakati wapenzi wanaposhiriki kitendo cha ndoa," Dkt Kibe alisema.


Daktari huyo alisema wale ambao hunyoa nywele hizo wanahatarisha maisha yao kwani ni rahisi kuambukiwa magonjwa ya zinaa.



Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipoBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini