Ruge Mutahaba Amezikwa Kishujaa Kijijini Kwao Kiziri, Bukoka

Aliyekuwa mkurugenzi wa vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba amezikwa kishujaa na idadi kubwa ya watu wakiwemo viongozi wa serikali ngazi mbalimbali, wasanii, taasisis binafsi na watu wenye vipawa tofauti kutoka ndani ya mkoa wa Kagera na nje ya mkoa huo.

Mazishi hayo yamefanyika leo Machi 4 huko kijijini kwao Kiziru, Bukoba huku mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group Joseph Kusaga akiahidi kuendeleza mazuri yaliyoachwa na Ruge Mutahaba.

Ameyasema hayo katika viwanja vya Gymkhana Bukoba wakati wakiaga mwili wa Marehemu Ruge Mutahaba na kisha kupumzishwa katika makao yake ya milele katika makaburi ya familia yaliyopo karibu na nyumba ya baba yake.

“Ruge alikuwa kinara wa mambo mengi mazuri alikuwa na talanta kubwa ya utunzi wa vipindi mbalimbali, Malkia wa nguvu, Kipepeo pamoja na Fursa ni baadhi ya vitu tutakavyo vienzi na kuviendeleza,” amesema Kusaga.

Mutahaba amefariki dunia Februari 26 Mwaka huu nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu baada ya kusumbuliwa na figo kwa muda. Ameacha watoto watano wanne wa kiume na mmoja wa Kike.




Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini