Tessy Chocolate Athibitisha Kumfutilia Mbali Aslay | ZamotoHabari.


Aliyekuwa Mpenzi wa Staa wa Bongo fleva Aslay Isihaka maarufu kama Aslay, Tessy Chocolate amethibitisha kumfutilia mbali staa huyo tangu Penzi lao  lilipoisha.

Miezi michache Baada ya Penzi hilo kufika mwisho Tessy Chocolate Amedai kwamba kwa sasa hapotezi muda wake kumu­waza mwanaume huyo, kwani ame­shamsahau na sasa ana maisha yake mengine.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Tessy alisema kuwa alipata shida mwanzoni lakini tangu agundue kwamba msanii huyo hakuwa chaguo lake alia­mua kuishi maisha yake.

Nilipata shida sana mwanzo­ni, kila mtu alikuwa ananishauri anavyojua yeye, lakini nashuku­ru Mungu siku zilienda na sasa hivi nimesham­sahau kabisa.

Kilichobaki kati yetu ni kumlea tu binti yetu Moza basi, pia sidhani kama naweza nikarudi tena kwake nina maisha yangu na ninayafu­rahia”.

Aslay na Tessy walikuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi kwa miaka mingi na wakafanikiwa kupata Mtoto mmoja wa kike anayejulikana Kama Mozah.
Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipoBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini