“Wote Wanaomkejeli Ruge Hawatamaliza Mwaka”- Mwijaku | ZamotoHabari.

“Wote Wanaomkejeli Ruge Hawatamaliza Mwaka”- Mwijaku
Muigizaji maarufu wa Bongo movie Mwijaku amewajia juu watu wote ambao wamekuwa wakimkejeli aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi Ruge Mutahaba.

Baada ya Ruge kufariki siku mbili zilizopita maneno Mengi yaliibuka kwenye Mitandao ya kijamii ikiwemo Msanii kama Dudubaya ambaye alianza kumuongelea vibaya Marehemu.


Baada ya watu Mbali Mbali kukemea Suala hilo Serikali imeingilia kati na sasa Hivi Msanii Dudubaya amewekwa chini ya ulinzi wa Polisi kwa muda usiojulikana.

Mwijaku amewajia juu watu wote wanaomsema vibaya Marehemu Ruge na kusema wazi kuwa yeye binafsi ana mpango wa kusali na kuwaombea dua watu wote ambao wanafanya matendo hayo na kuhakikisha kuwa watu hao hawatamaliza mwaka:

Naomba niseme kuwa mimi binafsi nitafunga na kusali na kufanya dua kwa ajili ya wote ambao wamekuwa wakimdhihaki Boss Ruge.

Mimi Ruge ni Kaka yangu kwaiyo hiyo Dua naapa itawafikia hao watu na ninawahakikishia hao watu kuwa huu mwaka hawataumaliza “.


Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipoBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini