ZOEZI LA UTOAJI ELIMU UNAENDELEA KWA WASAFIRISHAJI MKOANI MBEYA | ZamotoHabari

 Mkuu wa Kitengo cha Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Julius Chambo, akitoa elimu kwa madereva wa malori kuhusu utekelezaji wa Sheria mpya ya Udhibiti wa Uzito wa Magari ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, mjini Tunduma, mkoani Mbeya. Sheria hiyo imeshaanza kutumika tarehe 1 Machi, 2019.
 Dereva wa malori ya mizigo Bw. Juma Nachikolo, akiuliza swali kwa Mkuu wa Kitengo cha Usalama na Mazingira kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Julius Chambo (hayupo pichani), mara baada ya kupewa elimu ya Sheria mpya ya Udhibiti wa Uzito wa Magari ya Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyoanza kutumika tarehe 1 Machi, 2019, mjini Tunduma, mkoani Mbeya.
Baadhi ya madereva wa malori wakisikiliza elimu inayotolewa juu ya utumikaji wa  Sheria mpya ya Udhibiti wa Uzito wa Magari ya Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyoanza kutumika tarehe 1 Machi, 2019.

Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipoBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini