CHADEMA WAMPOTEZEA JOSHUA NASSARI


Joshua Nassari

Uongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, umesema kuwa msimamo wao ni ule ule kwamba hautashiriki uchaguzi kwenye jimbo la aliyekuwa Mbunge wake Joshua Nassari, kutokana na sababu zao za awali kuwa hakuna uwanja sawa wa ushindani.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt Vincent Mashinji ambaye maamuzi ya kikao chao kilichofanyika hivi karibuni Jijini Dar es salaam kikiongozwa na Mwenyekiti wake Freeman Mbowe wameazimia kutoshiriki uchaguzi huo.

"Hatujabadili msimamo wa chama kutoshiriki chaguzi hizi, kwa sasa mtazamo wetu ni Uchaguzi Mkuu, na chama ndicho kinachoamua, kuhusu Nassari mwenyewe kama alikuwa ndani ya chama kwa ajili ya madaraka anaweza kuondoka”, amesema Dkt. Vicent Maashinji.

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini