Binti Auawa na Tembo Waliokuwa Wakifukuzwa Shambani | ZamotoHabari.

Tukio hili limetokea usiku katika kijiji cha Bukore kata ya Kyambahi, ambapo binti wa miaka 26, Motondi Shakanyi ameuawa kwa kushambuliwa na Tembo

-

Kaka wa marehemu amesema kuwa alitoka yeye na mdogo wake wa kiume kwenda kuwafukuza Tembo hao kwa kuwapigia madebe

-

Anasema alimsihi Mama yake na mdogo wake huyo wa kike wabaki nyumbani na wasitoke nje lakini baada ya muda na wao walitoka na kuanza kuwafuata

-

Wakiwa njiani ndipo walikutana na Tembo aliyemnyanyua binti huyo na kumtupa umbali wa mita 5 na alifariki papo hapo 


Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipo
BOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini