Serikali kushirikiana na TMRC katika ukopeshaji wa mikopo katika sekta ya nyumba. | ZamotoHabari.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

Serikali imesema kuwa litaendelea kushirikiana na Kampuni ya mikopo ya nyumba (TMRC) ambayo imeorodheshwa katika awamu ya pili katika hatifungani ya soko la Hisa Dar es Salaam (DSE).

Hayo ameyasema Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Khatib Kazungu katika hafla ya TMRC kuorodhoshwa hatifungani ya soko hilo iliofanyika jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa ni asilimia moja ya mikopo ya nyumba ikilinganishwa na nyingine hivyo wadau lazima waongeze jitihada ya kutoka hiyo asilimia moja na kuongeza zaidi ili wananchi kupata mikopo nyumba zenye riba nafuu.Amesema mpango wa ukopeshaji wa nyumba ulikuwa ukifanywa na Benki ya nyumba ambayo ilifisika na serikali kukopa katika benki ya Dunia na kuikopesha TMRC dola za kimarekani milioni 70.

"Serikali itaendelea kushirikiana wadau wote katika kukuza sekta ya nyumba nchi ikizingatiwa umuhimu wa umiliki wa nyumba" amesema Kazungu.Nae Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko na Dhamana na Mitaji (CMSA) Nicodemus Mkama amesema mauzo ya toleo la kwanza yalikamilika Juni 8 mwaka jana ambapo TMRC ilifanikiwa kukusanya billion 12 ikiwa ni asilimia 4.3 ambayo ni zaidi ya lengo lililokuwa limetarajiwa.

Amesema toleo la pili ya TMRC yamekuwa na mafanikio kwa sh.bilioni bilioni 9.2 ikilinganishwa na sh.bilioni nane zilizotarajiwa kukusanywa.

"Ongezeko hili linaonesha imani walionayo wawekezaji kwa Kampuni ya TMRC na CMSA na fedha zilizopatikana katika mauzo ya toleo la pili zitatumika kugharamia shughuli za maendeleo pamoja na kutoa mikopo yenye riba nafuu kwa benki zinazotoa mikopo ya nyumba"amesema Mkama.

Ametoa wito kwa mifuko ya hifadhi ya jamii na Taasisi za Fedha yatumie njia ya Masoko ya Mitaji ili kuongeza Ukwasi na uhakika zaidi.Kwa ipande wa Mwnyekiti wa Bodi ya TMRC Theobald Sabi amesema kuwa kwa imeshatoa mikopo kwenye benki 15 yenye thamani ya sh.bilioni 122.

TMRC iko katika mazungumzo na Taasisi za Kimataifa kwa ajili ya kupata mikopo nafuu ili mraji apate mikopo nafuu na riba.
 Mwenyikiti wa Bodi ya TMRC Theobald Sabi akitoa maelezo namna TMRC ilipopata mafanikio katika ukopeshaji wa mikopo ya nyumba katika Taasisi za Fedha na kuingia katika hatifungani ya kuorodhoshwa katika Soko la Hisa Dar es salaam awamu ya pili katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya Watendaji wakishuhudia kuorodhoshwa kwa TMRC  hatifungani awamu ya pili katika Soko la Hisa Dar es Salaam.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Khatib Kazungu akifungua Mnada katika Soko la His Dar es Salaam.
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Khatib Kazungu akizungumza wakati wa kuorodhoshwa kwa hatifungani ya kwa Kampuni ya mikopo ya nyumba TMRC katika Soko la Hisa Dar es Salaam awamu ya Pili hafla iliofanyika jijini Dar es Salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Dhamana na Mitaji (CMSA)   Nicodemus Mkama akitoa maelezo namna soko linavyopanda kwa Kampuni katika kuorodhoshwa kwa Hatifungani katika Soko la Hisa Dar es salaam  katika hafla ya TMRC kuorodhoshwa hatifungani awamu ya Pili katika Soko la Hisa Dar es Salaam (DSE).


Jiunge Grupu la Mishono ya Vitenge VITENGE MISHONO

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini