Serikali haitavumilia taasisi itakayokwamisha juhudi zake- Kangi Lugola | ZamotoHabari.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amesema kuwa Serikali ya Tanzania haitavumilia taasisi yeyote ambayo itaonyesha nia ya kukwamisha zoezi la kuwarejesha wakimbizi, wanaotokea nchi jirani ya Burundi.

Lugola ametoa kauli hiyo akiwa mkoani Kigoma alipotembelea kambi ya Wakimbizi Nduta, iliyopo wilayani Kibondo mkoani humo akiwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Burundi.

“Wakimbizi wa Burundi wanaoishi Tanzania, wanalelewa vizuri sana na mpango wa Serikali ni kuwarejesha nyumbani kwao Burundi, kwa kuwa sasa kuna amani.”amesema Lugola

Aidha, Waziri Lugola amesema Serikali katika kila wiki itakuwa ikiwarudisha wakimbizi 2000 mpaka pale watakapoisha.
Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipo
BOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini