Aliyefariki kwa Ugonjwa wa Corona Kuzikwa Leo na Serikali ni Mdogo wa Bregedia Generali Mbita | ZamotoHabari.


Familia ya Marehemu Alhaj Brigedia Generali Hashim Mbita kwa huzuni kubwa inasikitika kutangaza msiba wa mdogo wao mpendwa Iddi Hashim Mbita aliyefariki usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Mloganzila kwa ugonjwa wa Corona.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na familia hiyo imeeleza kuwa serikali itamzika leo mchana.

“Kutokana na tatizo lililopelekea kifo chake Corona serikali itamzika mpendwa wetu leo mchana. Wawakilishi wachache sana wa familia wataruhusiwa kuhudhuria mazishi,” taarifa hiyo imeeleza


Aliyefariki kwa Corona Iddi Hashim Mbita
Taarifa hiyo imeeleza kuwa hakutakuwa na msiba wala matanga ya pamoja kuepuka kueneza maambukizi.

“Kila mtu aomboleze kwake.
Dua nyingi tumuombee Iddi Allah amuweke pema peponi. Amina,” taarifa hiyo imeeleza.

APP YETU MPYA: Sasa unaweza kusoma kwa urahisi kupitia APP yetu. Download hapa kwa KUBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini