CORONA: Wafanyakazi wa UN Kufanyia Kazi Nyumbani | ZamotoHabari.



Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, amewaagiza wafanyakazi wote wa makao makuu ya umoja huo kufanyia kazi nyumbani kwa muda wa mwezi mmoja ili kuepuka maambukizi ya virusi vya corona.

Amesema kuanzia machi 16 hadi Aprili 12 mwaka huu, wafanyakazi wote wa makao makuu ya umoja huo huko New York nchini Marekani watafanyia kazi zao nyumbani isipokuwa tu kwa watakaopata dharura itakayowalazimu kufika ofisini.

Guterres ametoa agizo hilo baada ya mwanadiplomasia wa Ufilipino anayefanyakazi katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kuthibitika kuambukizwa virusi vya corona.

Mwanadiplomasia huyo alikuwa ameshiriki moja ya vikao vya Umoja wa Mataifa.

Wakati huo huo, Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa kuanzia machi 16 hadi mwisho wa mwezi Aprili mwaka huu, vikao vingi vilivyokuwa vifanyike kwenye makao makuu ya umoja huo navyo vimesitishwa.

Kampuni mbalimbali na mashirika mengi likiwemo lile la Fedha Duniani (IMF) yamerudisha wafanyakazi wao nyumbani, lengo likiwa ni kukabiliana na maambukizi ya virusi vya corona.

APP YETU MPYA: Sasa unaweza kusoma kwa urahisi kupitia APP yetu. Download hapa kwa KUBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini