Serikali ya Guinea yasema ugonjwa wa corona hautazuia uchaguzi | ZamotoHabari.

Serikali ya Guinea-Conakry imesisitiza kufanyika kwa uchaguzi wa wabunge na kura ya maoni ya katiba pamoja na kuwa wapinzani wanataka uchaguzi usitishwe kutokana na hofu ya kuenea ugonjwa wa COVID-19 au corona.

Aidha wapinzani wanautazama uchaguzi huo ambao utafanyika kesho Jumapili kuwa mbinu za rais Alpha Condé ambaye anataka kubadilisha katiba ili aweze kuwania muhula wa tatu kinyume cha sheria ya sasa.

Ingawa katiba mpya ambayo inatazamiwa kuidhinishwa katika kura ya maoni ina kipengee cha mihula miwili ya rais ambayo sasa imeongezwa kutoka miaka mitano hadi miaka saba, lakini rais Conde amesema mihula yake iliyopita haipaswi kuzingatiwa na hivyo anaweza kugombea mihula mingine miwili.

Serikali imesisitiza kuwa hakuna uwezekano wa kuahirishwa matukio hayo muhimu kwa nchi na maandalizi yanaendelea vizuri licha ya janga la Covid-19 ambalo Guinea imethibitisha kesi mbili za maambukizi ya kirusi cha ugonjwa huo.
 


APP YETU MPYA: Sasa unaweza kusoma kwa urahisi kupitia APP yetu. Download hapa kwa KUBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini