Eto'o Awajia Juu Maprofesa Wa Ulaya kuhusu chanjo ya COVID-19 kufanyiwa majaribio Afrika | ZamotoHabari.


Supastaa wa zamani wa Inter Milan na Chelsea, Samuel Eto'o amewatolea uvivu maprofesa nchini Ufaransa kufuatia matamshi yao yasiyofaa juu ya Afrika kipindi hiki ambacho ulimwengu unatafuta ufumbuzi dhidi ya kupambana na ugonjwa wa Virusi vya Corona.

Hakuna dawa ambazo zinaweza kuzuia ugonjwa huu, lakini wanasayansi wamegundua chanjo ya BCG, inayotumika kupunguza makali ya ugonjwa huo.

Kupitia kituo cha televisheni cha Ufaransa LCI, Profesa Jean-Paul Mira, mkuu wa kitengo cha huduma ya wagonjwa katika hospitali ya Cochin (Paris) na Profesa Camille Locht, mkurugenzi wa utafiti huko Inserm alipendekeza ufanisi wa chanjo hiyo inapaswa kufanyiwa majaribio Afrika.

Kauli hiyo, ilimchukiza Eto'o na kutumia mtandao wake wa kijamii kwa kuandika. "Afrika sio uwanja wako wa kucheza."

Nyota wa kimataifa wa Senagel, Demba Ba, alionekana kukerwa na msomi huyo kwa kuandika, "Karibu Magharibi, ambapo watu weupe wanajiamini kuwa bora zaidi kwamba ubaguzi wa rangi na ujasusi huwa kawaida. Wakati wa kuinuka."

Kiungo wa zamani wa Ufaransa na kiungo wa Inter Milan, Olivier Dacourt alionyesha msimamo wake katika Twitter.

"Je! Ni kweli wapo siriazi?" aliuliza.

Kuna watu wamekuwa wakikimbilia Ulaya ili wasaidiwe kisiasa lakini hivi ndivyo wazungu wanavyotuchukulia




APP YETU MPYA: Sasa unaweza kusoma kwa urahisi kupitia APP yetu. Download hapa kwa KUBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini