Kenya yapiga marufuku usafiri katika miji iliyoathirika na virusi vya corona | ZamotoHabari.


Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta jana ametangaza kusitishwa kwa safari zote katika maeneo yaliyoathirika na virusi vya corona nchini humo.

Katika hotuba aliyoitoa , Kenyatta ametaka kusitishwa kwa usafiri wote wa umma kwa njia ya barabara, reli na hata ndege katika kaunti ya Nairobi, Mombasa, Kilifi na Kwale kwa siku ishirini na moja ili kukabiliana na maambukizi ya virusi vya corona.

Marufuku hayo yameanza kutekelezwa jana saa moja jioni  huko Nairobi na kuanzia siku ya Jumatano huko Mombasa, Kilifi na Kwale.

Hapo awali rais Uhuru alitangaza marufuku ya nchi nzima ya kutotoka nje usiku ila maambukizi yanaonekana kuongezeka huku visa vya maambukizi vikifikia 158 baada ya kuripotiwa visa vyengine sita jana.

Idadi ya waliofariki kutokana na virusi hivyo imeongezeka pia na kufikia watu sita.

APP YETU MPYA: Sasa unaweza kusoma kwa urahisi kupitia APP yetu. Download hapa kwa KUBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini