Lulu Michael Afunguka Kuitamani Ndoa...... | ZamotoHabari.



MWIGIZAJI wa fi lamu nchini Elizabeth Michael ‘Lulu’ amesema kuwa alitamani sana kuwa na mtoto alipofi kisha umri wa miaka 22.


Mrembo huyo alisema ingawa hadi sasa bado hajafanikiwa ila anaamini ukifika wakati wa Mwenyenzi Mungu atajaliwa kupata mtoto wake.


“Sikuwahi kuwaza kuolewa, ila nilitamani niwe na mtoto wangu nikiwa na miaka 22, nilitamani sana kuzaa, lakini mipango ya mwanadamu sio mipango ya Mungu, nina miaka 25 sasa na bado sijajaliwa mtoto, naamini wakati wa Bwana ukifika nitazaa,”alisema.



Lulu aliwahi kuvishwa pete ya uchumba na Francis Ciza maarufu kama Majizzo mwishoni mwa Septemba 2018 na mpaka sasa hakuna ndoa iliyofungika.



APP YETU MPYA: Sasa unaweza kusoma kwa urahisi kupitia APP yetu. Download hapa kwa KUBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini