Na. John Mapepele
Tamasha la Muziki la Serengeti leo Machi 13, 2022 linaingia katika siku yake ya pili na ya mwisho katika viwanja wa Chinangali jijini Dodoma baada ya kazi nzuri ya jana huku msanii nguli Harmonize kuwa miongoni mwa wasanii wataopanda jukwaani.
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amewataka wasanii waliopata fursa kushiriki katika tamasha hili kutoa burudani kabambe ili kuonyesha vipaji vyao na kuitangaza Tanzania.
Wasanii waliopanda jana waliwapagawisha mamia ya wapenzi waliofurika kuwaburudisha kutokana na umahiri wao wa kutumbuiza, huku wengine wakifanya kolabo kama AY na Mbunge wa Muheza na Msanii Mkongwe Mwana FA na kuwa miongoni mwa vivutio katika tamasha hili.
Kundi la wasanii machachali na chipukizi wataungana na wakongwe ambao watahitimisha tamasha la mwaka huu leo Machi 13, 2022 kwa kiingilio cha shilingi 3000 getini.
Mbali na wasanii wengi watakao burudisha leo Ma Dj wakongwe wanatarajia kutawala jukwaa kwa vionjo vyao.
Kutokana na uratibu nzuri wa tamasha hili ambalo limeratibiwa na Serikali kupitia Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na wadau kumekuwa na shauku kubwa kwa Wasanii mbalimbali kufanya vizuri ili waweze kuinua viwango vyao.
Jana wakati Wasanii wakitumbuiza Serikali kupitia kwa Waziri Mkuu. Mhe Kassim Majaliwa ilitoa msimamo wa kuendelea kuandaa na kuboresha tamasha ili kuendelea kutumia sanaa kuitangaza Tanzania kimataifa.
Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipoBOFYA HAPA
0 Comments