TUNAIWAZA ROBO FAINALI KULIKO KITU CHOCHOTE - AHMED ALLY | ZamotoHabari


Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV

Wawakilishi pekee kwenye Michuano ya Kimataifa, ngazi ya Klabu, Simba SC wikiendi hii, Aprili 3, 2022 watakutana na timu ya USGN ya Niger katika mchezo wa Kundi D la Kombe la Shirikisho barani Afrika, mchezo utakaopigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu hiyo, Ahmed Ally amesema wamejipanga kufanya vizuri katika mchezo huo kuhakikisha wanafuzu hatua ya Robo Fainali ya Michuano hiyo, amesema wanataka zaidi kufuzu hatua hiyo kuliko kitu chochote.

“Tunaingia kwenye mchezo wetu dhidi ya USGN, tukiwa tumejiandaa kufanya vizuri ili tufuzu Robo Fainali ya Michuano ya Kombe la Shirikisho. Tunashukuru hadi sasa tuna majeruhi mmoja tu, ambaye ni Hassan Dilunga, lakini Sadio Kanoute amerejea tayari Kikosini licha na yeye kutoka kwenye majeruhi”, ameeleza Ahmed.

Pia ameeleza kuwa Simba SC imejifunza kuwa makini katika michezo muhimu zaidi, tangu ilipotolewa na UD Songo ya Msumbiji na Jwaneng Galaxy FC ya Botswana ambao waliwatoa kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika katika hatua muhimu ikiwa hatua ya kufuzu makundi.

“Wachezaji wetu wanajua nini kipo nyuma yao, wanajua nini Wanasimba wanahitaji, wanajua mchezo huo ni muhimu kuhakikisha tunafuzu Robo Fainali ya Michuano hiyo”, amesema Ahmed.

Union Sportive Gendarmerie Nationale wanatarajiwa kutua siku ya Alhamisi, Machi 31, 2022 kwa ajili ya mchezo huo dhidi ya Simba SC. Mwamuzi wa mchezo huo anatarajiwa kuwa Helder Martins kutoka nchini Angola.


 

Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipoBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini