SAID CHINO BINGWA MPYA WA IBA INTERNATIONAL | ZamotoHabari

 Historia imeandikwa Tanzania, baada ya Mkanda mwingine kubakia katika Ardhi ya Tanzania ambaoo Bondia Said Mohamed maarufu kama Said Chino kuwa bingwa mpya wa IBA Intercontinental Championship kwa kumchapa mpinzani wake raia wa Afrika Kusini Lusanda Komanisa kwa pointi.

Said Chino ameshinda pambani hilo kwa point kutoka kwa majaji wote watatu

Kwa ushindi huo Said Mohamed amezwadia #KnockoutyaMama ya Shilingi milioni tano kama zawadi , ambapo katibu mkuu wa Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo Gerson Msigwa amesema kuwa Mhe Rais Samia Suluhu Hassan ameamua kuisapoti sekta yote ya michezo na kwasasa mapambano yote ya kimataifa yatakayohusisha mabondia wa Kitanzania basi Mh. Rais Samia atakuwa motisha kwa mabondia hao









#KnockoutyaMAMA



Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipoBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini