IDARA KUU YA MAENDELEO YA JAMII YATAKIWA KURATIBU SHUGHULI NA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI NCHINI

akiingia

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Watoto Dokta Faustine Ndugulile akiwasili Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii wakati alipofanya ziara kwa mara ya kwanza.

akiongea watumishi

Sehemu ya Watumishi wa Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya.

akiongea

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Watoto Dokta Faustine Ndugulile akizungumza na watumishi wa Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii wakati alipofanya ziara kwa mara ya kwanza.

akipokea ua

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Watoto Dokta Faustine Ndugulile akikabidhiwa ua na Afisa Utumishi Bi. Daina Lumelezi wakati alipotembelea Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii.

wakiongea

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Watoto Dokta Faustine Ndugulile akibadilishana mawazo na viongozi wa Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii mara baada ya kumaliza kuzungumza na watumishi wakati alipofanya ziara kwa mara ya kwanza.

watumishiMsajili

Msajili wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali Bw. Marcel Katembo akizungumza wakati wa kikao baina ya Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia wanawake na Watoto.

picha pamoja

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Watoto Dokta Faustine Ndugulile akiwa katika picha ya pamoja na viongozi pamoja na watumishi wa Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii wakati alipofanya ziara kwa mara ya kwanza. PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO WAMJWW

…………………………………………………………………

Na WAMJWW

Naibu Waziri wa Afya Maendelo ya Jamii jinsia Wanawake na Watoto Dokta Faustine  Ndugulile ameitaka Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii  kuratibu shughuli znazofanywa na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali  ili yafanye kazi kulingana na uanzishwaji wa mashirika hayo.

Dokta Ndugulile aliyasema hayo jijini Dar es Salaam  wakati akizungumza na watumishi wa Wizara ya Afya Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii  alipokwenda kujitambulisha kufuatia kuteuliwa  hivi karibunoi  katika mabadiliko yaliyofanyika  ya baraza la mawaziri.

Alisema , pamoja na idara hiyo kuwa na kanzi data kwa ajili ya mashirika yasiyo ya kiserikali nchini lakini kuna haja ya kufuatilia utendaji  kazi wa mashirika yasiyo ya kiserikali kwani  baadhi ya mashirika hayo yamekuwa yakienda kinyume na kazi iliyokusudiwa.

‘”kuna mashirika yasiyo ya kiserikali ya Kimataiafa na yale ya kitaifa ni vizuri yale ya kimataifa yawe na sura ya kimataifa nay ale yenye sura za kitaifa yabaki na sura hiyo  kwani wakati mwingine hasa kipindi cha uchaguzi  baadhi ya mashirika hayo hujishughulisha na shughuli za kisiasa na kuacha malengo ya kuanzishwa kwake’’.

Aidha, dokta Ndugulile ameenda mbali zaidi kwa kusema baadhi ya mashirika yasiyo ya kiserikali  yamekuwa yakijishughulisha pia na masuala  yanayoenda kinyume na maadili ya Tanzania hivyo amaitaka idara hiyo ihakikishe kila shirika lisilo la kiserikali linatumia fedha  inazopatiwa kwa malengo yaliyokusudiwa.

Akizungumzia suala la huduma za jamii kwa wazee, Dk Ndugulile alisema, pamoja na jitihada zinazofanyika katika kuwahudumia wazee bado eneo hilo lina changamoto kubwa hususan  katika misamaha ya kuhudumia wazee  katika huduma za afya pamoja na nyumba za kuwatunza wazee.

Alisema katika vituo vya kuhifadhia wazee kumekuwa na changaomoto nyingi na wakati mwingine kulazimu vituo hivyo kusaidiwa na watu  wengine tofauti na idara husika katika huduma mbalimbali kama vile huduma za umeme.

Aidha, ameshauri kupitiwa upya kwa Sera, Sheria na Miongozo ya Idara kuu ya maendeleo ya jamii kwa kuwa sera Sheria na miongozi iliyopo haendanane na wakati uliopo sasa.

Amewataka watumishi wa Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii kuwa wabunifu kwa rasilimali chache zilizopo na kufanya tafiti wakati wa kufanya kazi zao na kusisitiza kuwa asingependa watumishi watofautiane naye katika ufuatiliaje wa shughuli za Wizara.

Hivi karibuni Wizara ya Afya kupitia Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii iliendesha zoezi la la kuhakiki mashirika yasiyo ya kiserikali kwa lengo la kuhuisha orodha ya mashirika hayo na kuboresha kanzi data ili kupima utekelezaji wa majukumu ya mashirika hayo.


Sponsored by ZAMOTO MEDIA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini