KLABU YA YANGA YAJIANDAA KUTISA DUNIA KWENYE MICHUANO YA MABINGWA YA AFRIKA,,NSAJIGWA ATOA YA MOYONI,SOMA HAPO KUJUA

Yanga imeonekana kupania kufika mbali kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kutuma baadhi ya wawakilishi nchini Shelisheli kwa ajili ya kuwaangalia wapinzani wao, St Louis.

Kauli hiyo, aliitoa kocha msaidizi wa timu hiyo, Shadrack Nsajigwa muda mfupi mara baada ya kumalizika kwa mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Mwadui FC ambayo ilimalizika kwa suluhu.

Yanga wanatarajiwa kuanza kucheza mchezo wao wa kwanza dhidi wapinzani wao St Louis kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam mnamo Februari 27 kisha kurudiana ugenini.

“Tahadhari muhimu tunapoelekea katika michuano hii mikubwa Afrika imeshaanza kuchukuliwa, tumeanza mapema mikakati hiyo ya kutuma wawakilishi wetu watakaoifuatilia kwa ukaribu St Louis kwa kujua mbinu wanazozitumia wakiwa uwanjani, pia wachezaji hatari wa kuchungwa.

“Kingine ni kwenda kuandaa mazingira ya hoteli kabla ya timu kwenda huko katika mechi ya marudiano kama unavyofahamu fitna zinakuwa nyingi katika michuano hii,” alisema Nsajigwa. 

Sponsored by ZAMOTO MEDIA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini