Vinara wa ligi kuu soka Nchini england klabu ya Manchester City jana usiku ilitinga katika hatua ya Robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya licha ya kufungwa nyumbani bao 2-1 na FC Basel ya Uswiss Manchester City iliingia kwenye mchezo wa jana ikiwa tayari na kumbukumbu nzuri ya ushindi wa bao 4-0 walioupata ugenini ambao umewafanya kufuzu hatua ya Robo fainali kwa ushindi wa jumla wa bao 5-2. Gabriel Jesus ndiye aliyeifungia Manchester City bao pekee katika mchezo wa jana huku FC Basel wakipata mabao yao kupitia kwa Mohamed Elyounoussi na Michael lang.
Sponsored by ZAMOTO MEDIA
0 Comments