SERENGETI BOYS YAANZA MICHUANO YA UEFA ASSIST,YAKUNWA GOLI 1-0 DHIDI YA GUINEA. | ZamotoHabari


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

KIKOSI cha vijana chini ya miaka 17 Serengeti Boys kimeanza michuano ya UEFA Assist kwa kukubali kufungwa goli 1-0 dhidi ya wapinzani wao Guinea.

Mchezo huo wa kwanza kwa Serengeti Boys ulichezwa kwenye Uwanja wa Emri Complex, huku mvua kubwa ikiwa inanyesha.

Katika mchezo huo, kipindi cha kwanza kilionekana kutawaliwa zaidi na wapinzani wao Guinea na wakatumia udhaifu wa safu ya ulinzi ya Serengeti Boys pamoja na golikipa kupata goli la kuongoza.

Safu ya ushambuliaji ya Serengeti Boys ilishindwa kuwa na maelewano mazuri na kushindwa kuwa na mipango ya kusawazisha goli hilo.Mpaka mpira huo unaenda mapumziko Serengeti Boys walitoka wakiwa nyuma kwa goli moja dhidi ya Guinea.

Kipindi cha pili kilianza na Serengeti Boys wakionekana kupata uhai na kutaka kutafuta goli la kusawazisha ila kujiamini kwa wachezaji wa Guinea kilizidi kuwapa wakati mgumu vijana wa Serengeti na kupoteza nafasi nyingi za kufunga.

Wachezaji wToure Alya na Mohamed Lamine wa Guinea walitawala nafasi ya kiungo na kuipa Serengeti wakati mgumu.Hata hivyo, baada ya Lamine kutolewa katika kipindi cha pili, ilitoa nafasi kwa Serengeti kufanya vema zaidi na kutawala huku ikipoteza nafasi kadhaa za kufunga.

Serengeti Boys itashuka dimbani tena keshokutwa Jumatano kuwavaa Australia katika mechi ya pili ya Kundi Namba Moja itakayopigwa saa 9:30 Alasiri kwa muda wa Afrika Mashariki.

Mechi ya mwisho ya Serengeti Boys itakuwa dhidi ya wenyeji Uturuki. Serengeti wapo katika michuano hiyo ikiwa ni maandalizi ya kujianda na michuano ya mataifa Afrika kwa vijana yanayofanyika hapa nchini mwezi April mwaka huu.
KIKOSI cha vijana chini ya miaka 17 Serengeti Boys


Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipoBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini