KATIBU MKUU UVCCM TAIFA AZINDUA KONGAMANO LA MTWARA YA KIJANI KWA KISHINDO | ZamotoHabari.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mwl Raymond Mwangwala leo amezindua rasmi Kongamano ya Mtwara ya Kijani lililofanyika katika Uwanja wa Nangwanda Mkoa wa Mtwara.

Akizungumza na Maelfu ya Wananchi waliohudhuria Ufunguzi huo Katibu Mkuu Mwl Mwangwala amewataka Kuendelea kukiamini Chama cha Mapinduzi kwani ndio Chama pekee kisichokuwa na Misingi ya Kiubaguzi wa Matabaka mbalimbali.

Pia, Katibu Mkuu Ndugu Mwl Raymond Mwangwala akizungumza katika Mkutano huo ametuma salama kwa Viongozi mbalimbali wa Vyama vya Upinzani kujiandaa kuachia ngazi kwani hakuna mwananchi wa sasa atakae acha kuipigia kura CCM kutokana na kasi ya Utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi inavyotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.

Aidha, Ndg Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa amewapongeza Viongozi wa Umoja wa Vijana wa Mkoa wa Mtwara kwa Kazi kubwa wanayoifanya ya kuendelea kuwa karibu na kuwasaidia Vijana wote wa Mkoa huo kuendelea kutatua Changamoto zao kwa kutimiza moja ya lengo la kuundwa kwa  jumuiya hiyo.

Akizungumza awali akimkaribisha mgeni rasmi Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Mtwara Ndugu Yusuph Nanila amemuhakikishia mgeni rasmi hali ya Kisiasa ya Chama na Serikali Mkoa wa Mtwara ipo vizuri na kutumia fursa hiyo kuwapongeza Watumishi mbalimbali wa Serikali wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa Mhe Gelasius Byakanwa  kwa kuendelea kuwatumikia Wananchi kwa Haki na Usawa.
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mwl Raymond Mwangwala akiwasili katika uwanja wa Uwanja wa Nangwanda Mkoa wa Mtwara kuzindua rasmi Kongamano la Mtwara ya Kijani . 
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mwl Raymond Mwangwala akizungumza mbele ya Wananchi waliohudhuria Ufunguzi huo 




Jiunge Grupu la Mishono ya Vitenge VITENGE MISHONO

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini