Mrithi' wa Tundu Lissu Aapishwa Rasmi, mahakama kutoa uamuzi Septemba 9 | ZamotoHabari.

Miraji Mtaturu, kutoka Chama Cha Mapinduzi, CCM, ameapishwa rasmi hii leo kuwa mbunge wa Singida Mashariki.

Mtaturu anachukua kiti hicho cha ubunge ambaho awali kilishikiliwa na Tundu Lissu aliyevuliwa ubunge wake na Spika Job Ndugai mnamo Juni 28 mwaka huu.

Tundu Lissu amekuwa nchini Ubelgiji akipokea matibabu baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana mchana wa Septemba 7 mwaka 2017.

Lakini wakati akiwa huko Spika Ndugai alimvua ubunge kwa madai kwamba hakuwa ametoa taarifa rasmi ya alipo, na pia hakuwa amejaza fomu za mali na madeni ya viongozi wa umma.

Israel na Hezbollah: Zaelekea vitani?
Magufuli: ' Vijana siku hizi wanapenda wanawake wenye magari'
Mtaturu alitangazwa mbunge mteule wa jimbo hilo kwa kupita bila ya kupingwa katika hatua za awali za matayarisho ya uchaguzi mdogo baada ya wagombea 12 wa vyama vya upinzani kutorejesha fomu.

Uchaguzi huo mdogo ulikuwa ufanyike Julai 31, lakini haukufanyika tena kutokana na wapinzani kutokurejesha fomu zao.

Hata hivyo, kuna kesi mahakamani ambayo inaweza kuathiri kiapo cha Mtaturu hii leo pale ambapo maamuzi yake yatakapotolewa wiki ijayo.

Kesi hiyo imepelekwa mahakamani na Lissu akipinga kuvuliwa ubunge wake.

Yalijoriri mahakamani jana
Hapo jana mawakili wa Lissu walitarajia kuzuia kuapishwa kwa Mtaturu hii leo hadi pale kesi hiyo itakaposikizwa na kuamuliwa.

Hata hivyo, Jaji Sirillius Matupa wa Mahakama Kuu ya Tanzania alilikataa ombi hilo la mawakili wa Lissu akisema katika kesi za ubunge hata kama mtu ameapishwa anaweza kuvuliwa ubunge pamoja na kiapo chake.

Kesi hiyo hapo jana iliunguuma mpaka saa tatu kasoro robo usiku ambapo Jaji alitangaza maamuzi yake juu ya ombi la kiapo cha Mtaturu.

Jaji Matupa amesema kuhusu maombi rasmi ya Lissu kupinga kuondolewa katika ubunge yatatolewa Septemba 9, 2019.

Image caption
Tundu Lissu anapinga mahakamani kuvuliwa ubunge na Spika Job Ndugai
Lissu amefungua maombi chini ya hati ya dharura, kupitia kwa kaka yake Alute Mughwai, ambaye amempa mamlaka ya kisheria kufanya hivyo, akitaka kurudishiwa ubunge wake.

Lissu anapinga vikali kuvuliwa wadhifa wake akidai kuwa amefutwa ubunge huku ikifahamika wazi kuwa amekuwa nje kwa matibabu tangu tarehe 7 mwezi Septemba mwaka 2017, baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana.

Mwanasiasa huyo hapo awali aliiambia BBC kuwa alitarajia hatua zilizochukuliwa na Spika dhidi yake kwa sababu alishasema kwa hiyo ilipotokea mwezi wa sita wala haikuwa ajabu.

''Mtu ambaye alishakuwa na nia ya kunifuta ubunge nisingeweza kumzuia, vinginevyo labda ningesema niachane na habari ya matibabu nirudi Tanzania''.
Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipo
BOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini