Mzozo wa meli ya Iran: Mafuta yauzwa licha ya vitisha vya Marekani | ZamotoHabari.

Meli ya mafuta iliyokuwa ikishukiwa kujaribu kufikisha mafuta ya Iran nchini Syria licha ya vikwazo vya kimataifa hatimaye imeuza shehena iliyokuwa ikisafirisha.

Picha za satelaiti zinaonesha kuwa meli hiyo Adrian Darya-1, ilikuwa karibu na pwani ya Syria mpaka Ijumaa.

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Iran hata hivyo amesema meli hizo imefikisha mzigo baada ya kutia nanga kwenye "pwani ya bahari ya Meditterania."

Meli hiyo imekuwa katikati ya mzozo wa kidiplomasia baina ya Marekani na Iran, na ilikuwa imebeba shehena ya mapipa milioni 2.1 ya mafuta.

Picha za Setilaiti zilitolewa na kampuni ya Maxar ambazo ilisema kuwa zilionyesha eneo la Adrian Darya maili kadhaa kwenye ufukwe wa badanri ya Syria wa Tartus Ijumaa.

Haki miliki ya pichaMAXAR'S TECHNOLOHIES
Ilikamatwa na wanajeshi wa Uingereza karibu na pwani ya Giblatar mwezi Julai na kushikiliwa mpaka Agosti 15 baada ya Iran kutoa hakikisho kuwa meli hiyo haitaelekea Syria.

Marekani imeshatoa onyo la kumuwekea vikwazo vya kiuchumi yeyote atakayenunua mafuta hayo.

"Tutaendelea kuiwekea shinikizo Iran na kama Rais (Trump) alivyosema hakutakuwa na msamaha wa aina yeyote ka mafuta ya Iran," Afisa wa Hazina ya Marekani, Sigal Mandelker ameliambia shirika la habari la kimataifa la Reuters.
Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipo
BOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini