Corona yakwamisha kina Ester kupatiwa matibabu nje | ZamotoHabari.

 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kuwa kinaangalia namna ambayo itawawezesha kuwasafirisha Wabunge Ester Bulaya, Halima Mdee na Jesca Kishoa kwa ajili ya kupatiwa matibabu nje ya nchi kwa kuwa hali zao bado hazijatengemaa.


Akizungumza leo Machi 19, 2020, na EATV&EA Radio Digital, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Mambo ya Nje wa chama hicho, John Mrema amesema kuwa kulingana na hali ya maambukizi ya Virusi vya Corona ilivyo kwa sasa inawawia vigumu kuchukua maamuzi yoyote, kwakuwa nchi walizodhamiria kuwapeleka tayari zimekwishakumbwa na visa vya ugonjwa huo.

"Kina Ester wameruhusiwa juzi, isingekuwa Corona tulikuwa tunafikiria kuwapeleka nje kupata matibabu zaidi, lakini bado tunawaza nini cha kufanya, hali zao bado hazijatengemaa, hasa Ester aliyeumia ndani huwezi jua nini haswa kinasumbua, tulitaka kuwapeleka kwenye nchi ambazo zina matibabu mazuri kuliko sisi kama Kenya na Afrika Kusini" amesema Mrema.


APP YETU MPYA: Sasa unaweza kusoma kwa urahisi kupitia APP yetu. Download hapa kwa KUBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini