Ugonjwa wa corona wazidi kuenea Afrika, 800 waambukizwa | ZamotoHabari.


Kesi za maambukizi ya ugonjwa wa corona au COVID-19 barani Afrika zimepita 800 hadi kufikkia Ijumaa huku nchi mbalimbali zikiiimarisha hatua za kukabiliana na ugonjwa huo unaoenea kwa kasi kote duniani.

Kwa mara ya kwanza, Chad, Niger na Cape Verde zimeripoti kesi za maambukizi ya kirusi cha corona. Huko mashariki mwa Afrika, idadi ya watu waliothibitishwa kuambukizwa kirusi hicho ikiongezeka katika nchi za Tanzania, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Kwa mujibu wa taarifa aghlabu ya wagonjwa wa COVID-19 barani Afrika wametokea Ulaya na Marekani, na ili kuzuia ueneaji wa janga hili, nchi mbalimbali barani humo zimesimamisha safari za ndege kutoka nchi zilizokumbwa zaidi na janga hilo haswa nchi za Ulaya.
 


APP YETU MPYA: Sasa unaweza kusoma kwa urahisi kupitia APP yetu. Download hapa kwa KUBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini