Ebitoke Atibuana na Kitenge KISA Mwanamke 'Sijawahi Kuona Mshamba wa Mapenzi Kama Huyu" | ZamotoHabari.


Ebitoke
Kitenge na Ebitoke

Mchekeshaji Ebitoke ameonesha kuchukizwa na kitendo alichodai kufanyiwa na Mchekeshaji mwenzake Kitenge ambaye walikuwa na ukaribu wakuitana Dada na Kaka kutokana na kazi zao za vichekesho.

Ebitoke ameandika Kwenye page yake ya Instagram malalamiko yake dhidi ya Kitenge na kumdai harudishe fedha zake alizomuibia.

”Sijawahi kuoona kaka mpumbavu kama Kitenge na mshamba wa mapezi kama huyu nilijua naishi na ndugu yangu kumbe ni nyoka pamoja na undugu wote wewe ndio umekuwa snitch namba moja ndio maana hunenepi utaiishia hivyo hivyo
“Na hela zangu ulizoniibia kwenda kula bata na huyo precious_stellah utazirudishaa, ntaanika uchafu wako wote nimekuleta mjini mwenyewe unashoboka na huyo  precious_stellah Kumbe humjuw vizuri safari hii utarudi kijijini labda mimi sio Ebitoke” – Ebitoke


APP YETU MPYA: Sasa unaweza kusoma kwa urahisi kupitia APP yetu. Download hapa kwa KUBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini