Virusi vya Corona: Marekani yarekodi vifo vingi zaidi vya virusi vya corona kwa siku | ZamotoHabari.

Marekani imerekodi vifo vingi vya ugonjwa wa corona kwa siku huku watu 1,736 wakifariki siku ya Jumanne.

Idadi hiyo inaweka watu waliofariki kutokana na virusi hivyo nchini humo kufikia 12,722 kulingana na data za chuo kikuu cha Johns Hopkins.

Marekani ina wagonjwa 398,000 wa virusi hivyo waliothibitishwa , ikiwa ndio idadi kubwa zaidi duniani .

Visa vyote duniani vimepita watu milioni 1.4. Hatahivyo wakati wa mkutano na vyombo vya habari , rais Donald Trump alisema kwamba Marekani huenda inafikia kilele cha 'upinde'.

Wakati huohuo Mji wa Wuhan nchini China ambapo maambukizi yalianza umekamilisha amri yake ya kutengwa kwa wiki 11.

Takwimu mpya zilizotangazwa siku ya Jumanne zimepita rekodi ya awali iliokuwa na vifo 1,344 kwa siku nchini Marekani ambapo ilitokea tarehe 4 mwezi Aprili.

Idadi ya vifo inatarajiwa kupanda huku baadhi ya majimbo yakiwa bado hayajatoa takwimu zao za jumla.

Familia ya msanii wa Marekani John Prine imethibitisha kwamba msanii huyo alifariki kutokana na virusi hivyo vya corona.
 


APP YETU MPYA: Sasa unaweza kusoma kwa urahisi kupitia APP yetu. Download hapa kwa KUBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini