Tanasha Donna Atoa Siri Kuhusu Alivyopanga Kutoa Ujauzito wa Mondi ila... | ZamotoHabari.


Tanasha alisema kuwa hakutaka kumpenda Diamond hadi amjue vyema

Alieleza kuwa alishangazwa kujua kuwa alikuwa mja mzito pasi kutarajia

Alitaka kuavya mimba hiyo lakini baadaye akaamua kulea

Aliyekuwa kipenzi cha msanii Diamond Platnamz ambaye pia ni mama mwanawe, Tanasha Donna hatimaye amefunguka kuhusu jinsi mahusiano yake na Mondi yalivyokuwa haswa alipobaini kuwa ana uja uzito.

Kulingana Donna, hakuwa na mpango wowote wa kupata mtoto na msanii Mondi na kuwa habari kuhusu uja uzito wake uliamucha kinywa wazi.

Tanasha Donna clears the air on claims of smoking while pregnant

Katika mjadala na jarida la True Love, mama huyo wa mtoto wa kiume alieleza bayana kuwa alitaka kumjua Diamond kiundani kabla kupiga hatua kupata mtoto naye.

‘’ Nilijizuia dhidi ya kumpenda maana nilitaka kumjua kiundani. Nilishaa kugundua kuwa nilikuwa mjamzito. Sikuwa tayari kuwa mama. Ilifanyika maana sikuwa nazingatia kwa umakini kalenda yangu ya hedhi,’’ alisema.

What’s your all time fav Donnatella song? #petithrowback

”Nilifikiria kuhusu kuavya mimba na kujiahidi kuwa makini zaidi siku zijazo, nashukuru Mungu maana sikufanya nilivyofikiria,’’ Tanasha aliongezea.

Kulingana naye, Diamond alikuwa akimuuliza mara si haba iwapo angeweza kukubali kuolewa na msanii mwenza, kulingana naye washindani katika Sanaa.

Tanasha alijifungua mtoto wa Mondi na kumpa jina Naseeb Junior na bila shaka uhusiano wao ulipoisha, ndiye aliyekuwa naye kama kumbukumbu za Mondi kutoka Tanzania akifungua safari ya kurejea Kenya. Hii ni baada ya kumtema msanii huyo akimlaumu kwa visa vya mapenzi ya kando.

Hata baada ya kurudi Kenya, Donna ameonekana kusonga mbele na maisha kikamilifu bila kumbukumbu za Mondi hivi majuzi akitangaza wazi kuhusu jumba la kifahari alilojinunulia.

APP YETU MPYA: Sasa unaweza kusoma kwa urahisi kupitia APP yetu. Download hapa kwa KUBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini