Baada ya Uchebe Kufunguka Shulole Naye Afungua Mdomo " Kuhusu Maendeleo Yangu Mimi niko Sawa" | ZamotoHabari.



Baada ya lile 'seke seke' la kipigo kutoka kwa mumewe. Uchebe, Msanii/mjasiriamali Shilole ameandika " Salaam ndugu zangu,

Nimeona upendo, nimeona heshima na kukubalika kwa kiwango cha pekee katika wakati huu wa changamoto niliyokutana nayo.

Nashukuru sana kwa upendo wenu, Nashukuru sana wote walionijulia hali na kuniombea dua.

Kuhusu maendeleo yangu mimi niko sawa, naendelea kupambana. Changamoto ni sehemu ya maisha, haziwezi kunifanya nianguke. Lakini yote hayo sio kwa nguvu zangu, ni Mungu na upendo wa Watanzania wenzangu mnaonitakia mema.

Maisha yanaendelea, tuendelee kuijenga jamii yetu : Jamii itakayokataa kabisa unyanyasaji wa kijinsia.

APP YETU MPYA: Sasa unaweza kusoma kwa urahisi kupitia APP yetu. Download hapa kwa KUBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini