Bondia Cheka atwaa ubingwa wa UBO | ZamotoHabari.



Bondia wa Tanzania, Cosmas Cheka ameshinda pambano dhidi ya Mmalawi, Hannock Phiri lililofanyika Uwanja wa Jamhuri, Morogoro



Mabondia hao walipigana wa uzito wa Light kuwania UBO International Title ambapo pambano hilo lilikuwa la round 12.

Kwa uamuzi wa majaji ameonekana kushinda japo mpinzani wake ameonekana kutokubaliana na uamuzi huo wa kupoteza pigano hilo.

Mbali na hayo, Cheka amesema kuwa kama mpinzani wake hajaridhika, arudie pambano na kwamba yeye yuko tayari kumfuata Malawi.

Katika Mapambano ya utangulizi, Mwanadada Zulfa Macho, mtoto wa Yusuph Macho alishinda kwa Knock-Out kwenye round ya kwanza kwenye pambano dhidi ya Mmalawi, Ndau Chilimba

APP YETU MPYA: Sasa unaweza kusoma kwa urahisi kupitia APP yetu. Download hapa kwa KUBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini