Dudu Baya Ang'ang'aniwa Polisi Afunguliwa Jalada la matumizi mabaya ya mitandao | ZamotoHabari.

 Dudu Baya Ang'ang'aniwa Polisi Afunguliwa Jalada la matumizi mabaya ya mitandao
Jeshi la Polisi limefungua jalada la uchunguzi wa tuhuma za matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii dhidi ya msanii wa Bongo Fleva, Godifrey Tumaini a.k.a Dudu Baya.

Kamanda wa polisi Kinondoni, Mussa Taibu amesema wakijiridhisha na madai hayo, hatua nyingine za kisheria zitafuata.

Hatua hiyo ilifikiwa mara baada ya Dudu Baya kutumia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram kutoa lugha isiyofaa kimaadili kwa Marehemu Ruge.

Mapema jana Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt.Harrison Mwakyembe aliliagiza Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa kushirikiana na Polisi kuhakikisha wanamkamata Msanii DUDU BAYA kwa kosa la kukashifu na kutoa lugha za kejeli kwa Marehemu
Ruge Mutahaba.


Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipoBOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini