Lema Aliamsha DUDE Asema Kama Kuna Kiongozi Anaumwa Waseme na sio Kuficha | ZamotoHabari.


Mbunge wa Arusha mjini (Chadema), Godbless Lema amesema ujumbe aliouweka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda katika mtandao wa kijamii Twitter unaonyesha kuna jambo nchini.

Lema aliandika ujumbe huo kupitia ukurasa wake wa Twitter kuwa waache uwoga kama kuna mtu anaumwa ama kiongozi waseme kwani ni Mungu pekee ndiye hawezi kuumwa.

“Sio udhaifu mtu kuumwa ni udhaifu wa fikra kufikiri kiongozi hawezi kuugua,” aliandika Lema

Makonda katika ukurasa wake wa Twitter aliandika ujumbe kuwa usimuombee mabaya adui yako kwa sababu kuna siku utamhitaji. Tafakari.

Hata hivyo , Mbunge lema alimjibu kuwa ni kweli kabisa kwani adui wa nani kapatwa na mabaya?






Tembelea Website ya Nyimbo za Injili Africa. Pakua na Kusikiliza bure bila malipo
BOFYA HAPA

Post a Comment

0 Comments

close
Banner iklan disini